Karibuni katika blog ambayo itakuwa inaelezea mambo ya kinajimu (astrology), mawe ya bahati ya kinyota, matukio kinyota na kiutabiri, matukio kimataifa na kimataifa na wanaopenda kujifunza elimu hii, mafusho,kuongelea viumbe kama majini, malaika, mizimu, freemason na iluminat, tiba kwa njia ya vyakula na matunda, magonjwa kinajimu na tiba zake.

Wednesday, November 30, 2011

Watu wenye asili ya upepo na tabia zao

Watu wenye asili ya Upepo na tabia zao May 21- June 20 na September 23 - October 22 na January 20 - February 18, na watu wenye kuanziwa na herufi C, O, S,G, K, W au watu waliozaliwa tarehe 3, 7, 11, 15, 19, 23,27 na 31 au watu wenye sauti nzuri, wenye athari katika vifua vyao au migongo yao, watu wafupi wenye miguu minene,wenye kunyoa vipara au watu wenye rangi ya kuteleteza na wenye mikono myepesi au watu wenye vifua vya kutanuka, wenye mdomo ulio kolea weusi na pua yenye ubapa wenye macho ya kati kwa kati watu hawa tabia zao ni watu wanaopenda kusaidia watu, wanapenda kushauri wenzao pasipo wao kushauriwa na ni watu wenye kupata umaarufu na ni watu wenye kupenda kujishughulisha kibiashara na ni watu wenye kupenda kuwasaidia hata maadui zao pasina kujali ni wenye kubadilika badilika na wenye uamuzi wa haraka ni watu wenye kupendwa na watu kwani kazi wanazozifanya ni kazi kushawishi watu au za kuburudisha watu na pia hutegemewa na watu katika kazi zao na wana bahati ya kupendwa na wazazi wao na watu wenye kupenda kujipumzisha kwenye upepo na kipato chao ni chenye kubadilika badilika na ni watu wenye kupenda kusaidiwa na watu fulani na watu hawa mara nyingi huwa hawakai na mpenzi zaidi ya mmoja na hupendwa na wapenzi wasio wapenda wao, Kazi zao hutegemea majira na mara nyingi watu hawa hujishughulisha na shughuli za kuwaburudisha watu, wanapendeza kutoa hutuba na kujishughulisha na siasa na uamuzi wao wa haraka japo hubadilika badilika na ni watu wanaopatwa msongo wa mawazo na mapigo ya moyo kwenda kasi na huwa wnkazi ya ziada kuwaweka sawa wapenzi wao kwani wapenzi wao huhitaji ushauri kutoka kwao wakati mwingine watu hawa huwa ni watu wenye maringo, hupendelea mapambopambo,kujiajiri wao na hupata umaarufu kwa njia wasizozitegemea wao, na huwa na bahati ya kupata marafiki wengi wake kwa waume wakubwa kwa wadogo kutokana na tabia yao ya uaminifu na ukweli na watu hawa maadui zao wengi ni wenye nyota ya udongo kwani watu wa udongo hawapendi kusifia wenzao na hawa wanapenda kusifiwa na mungu huwajalia huishi maisha marefu.
Kazi za watu wa asili hii ni wanamziki,watangazaji,ufundi wa vyombo vya umeme, falsafa, uandishi,siasa, utumishi, kazi za serikali na hujishughulisha na biashara zao ambazo huwaletea matatizo, watu hawa wanabahati ya kukutana na wapenzi wenye asili ya moto na wapenzi wao hunyanyuka kwa kupitia wao, watu rangi zao za kinyota ni kijani kibichi, bluu bahari, kijivu,rangi ya fedha, njano watu hao wanashauriwa kutumia vyakula vyenye utamu utamu mfano matunda yenye asili ya unjano na utamu na wanashauriwa kutumia manukato yenye harufu nzuri wanashauriwa watu hawa kwani hukutana na watu mbalimbali na elimu yao huwasaidia kufika mbali. na nyota zao ni mapacha, mizani, ndoo.
Madini yao ni fedha, shaba, aluminium na mawe yao yawena asili ya ukijani, njano au rangi za kuvutia kwani nyota zao ni za kuvutia vile vile watu wa nyota hii wanashauriwa sana wakae sehemu za mwinuko au sehemu zenye uwanja mkubwa au pembezoni mwa mji watumie hizi kustarehe na wapenzi wao kwani wapenzi wao wa majanga utafutaji wa pesa unahitaji akili nyingi na utunzaji japo ni watu wa kutoa toa pesa hovyo. Mafusho ya nyota zao ni kachiri, mushtaka na miatusaila kwa watu wenye nyota ya ndoo na siku zao ni jumatano kwa mapacha, Jumamosi kwa ndoo na ijumaa kwa mizani kinyota watu hawa wanashauriwa kuwaunganisha marafiki kimapenzi kwani nyota zao ni nyota za kukusanya watu, wanashauriwa kuvaa nguo zenye kupendezesha na kwenda na wakati na mavazi yao mara nyingi yawe ni rangi moja na wanawake wao wanashauriwa kuvaa mapambo sana na viatu virefu, na wanawake wao wanashauriwa kutunza nywele japo hawapendi na mikoba wapende kuvaa. wanashauriwa watembe kwa mwendo wa madaha kwani huwafurahisha wapenzi wao na wapende kuwasemea sauti za chini na kuwaliwaza wawashike wapenzi wao vichwa,shingo zao na masikio yao na wawaminye minye mikono yao watawafurahisha wapenzi wao na washughulike sana wanapokuwa faraghani na wapenzi wao wawashe redio kwa sauti ya chini, muziki wa taratibu au nyimbo zenye kusikitisha na kuonewa, wawashe feni kidogo pembeni, na kwenye falagha wawasifie wapenzi wao kwani huwafurahisha na kuwapa chochote wanachotaka watu hawa  hupendwa na ndugu wa wapenzi wao.
Watu wenye asili hii kwa mwaka huu.
Watu wenye asili hii kwa mwaka huu maisha yao yamekuwa kawaida japo wamepoteza wapenzi wao waliowapenda sana na mwaka huu watu wa nyota hii wameanza kutafuta mali au jambo jipya japo linasuasua na mwaka huu wameandamwa na maradhi ya kutokujiamini na akili zao kufumba, na wamekutana na wapinzani wao katika shughuli zao wanashauriwa wakae na watu hao wasiowapenda kwani sasa hivi wanamatatizo wanahitaji msaada wa kifedha, kimali na kielimu kwani hao watu wasiowapenda ndio wanamsaada wao japo wa muda na sasa hivi watu hawa wanapenda kukaa kwenye makundi pasina maendeleo yoyote kuwashauri wenzao japo wenyewe wanamatatizo na mwaka huu wamepoteza kazi walizokuwa wanazitegemea na fani zao walizokuwa wanazitegemea zimeingia uzito kidogo, wawe makini kwani watu wanawaandalia kashfa ya uzinzi, pia watu hawa sasa hivi wanasumbuliwa na upepo wa ummu subiani ndio maana wakiamkaa huwa wanachoka na kutetemeka katika usingizi wao na kujihisi wavivu na ndoto mbaya, na hujihisi kuna kitu katika mgongo wake au kifua chake na huandamwa na hali za unyonge katika nafsi zao, wanashauriwa wawaone wazee wao wa dini wawafanyie dawa au maombi na kuondolewa upepo huo wa ummu subiani inshallah mungu atawasaidia.
Watu wenye asili hii kwa mwaka 2012.
Watu wenye asili hii ya upepo kwa mwaka huu utakuwa ni wenye faraja kwani kiu ya mambo yao yatakuwa na dalili ya kupatikana na maswala yao yaliyo kwama yatafunguka na wanauwezekano mkubwa wa kupata wapenzi wapya na wanashauriwa wawe makini katika maswala yao, wanashauriwa washirikiane na watu wenye asili ya moto au kiongozi fulani mkubwa wa kisiasa, kitamaduni na muda wao mzuri wa kujipanga katika elimu na mwaka wao mzuri wa kuanzisha mambo ya kisanaa watafanikiwa, wanashauriwa wasiende nchi za magharibi au magharibi kwani hawatofanikiwa jambo lao lolote. kimsingi watoe sadaka sana na wagawe vitu sana na wajitahidi kutafuta utatuzi wao wa uzazi na ni muda wao mzuri kuanza maisha yao mapya ya kifamilia au kindoa  hii ni kwa ufupi tu.
Nchi zenye asili ya upepo zitatawaliwa na jua na mvua zenye upepo mkali na wawe makini kwani kinaweza kutokea kimbunga chenye kuambatana na maji na nchi hizi zitashirikiana na nchi zenye maahasimu wao na zitapatikana suluhu katika migogoro yao na raisi na viongozi wengi watapatikana kwa njia ya halali kwani inaelekea kutakuwa na chaguzi nyingi katika nchi hizi na watatembelewa na viongozi wakubwa katika nchi kubwa na kutasikika habari ya wanamuziki, kuungana, kuoana katika dunia au kupata mali kwa msanii na watu wengi watapata ufahamu na kutagundulika baadhi ya siri zilizofichika kisiasa ili nchi hizi ziishi kwa amani na vyakula vya matunda vitakuwa vingi na nchi hizi zinashauriwa kujenga ujamaa na utulivu hii ni kwa kifupi tu.

Tuesday, November 29, 2011

Watu wenye asili ya moto na tabia zao

 Watu wenye asili ya moto na tabia zao Machi 21- April 19 na July 23- Augost 22 na November 22- December 21 na watu wanao anzia na herufi zifuatazo A, M, Y, E, Q,I, U. Hawa watu wana asili ya moto na kimaumbile ni watu wenye uso mwembamba, pua yenye kuchongoka, wenye vidole virefu vya mikono, na vidole virefu vya miguu, watu hawa wanatabia ya mambo ya haraka haraka, ni watu wenye hisia kali na wenye mipango mingi ya kitamaa na wenye kutumia akili zao katika utafutaji na watu wenye kupenda kuwazidi wenzao katika kifamilia na kikazi na ni watu wenye mbinu nyingi katika utafutaji wao hawaoni hasara kuharibu jambo alimradi watimize lao, na niwatu ambao huchemka akili zao wanapopata matatizo na hii huwaletea matatizo ya kupata ugonjwa wa kichwa, kuwaza sana, na kuwaletea ugomvi na ndugu zao wakubwa au wakike wenye uso wa duara na maziwa yaliyo tokeza.
Watu hawa hufanya kazi zenye asili ya moto au kudhibiti kama vyuma, magari, wanajeshi, walimu, na kazi zote zenye kuhusu akili nyingi na maamuzi.
Watu hawa wanashauriwa wasijiingize kwenye maswala ya kisiasa na ushindani ushindani wa kimaneno na kimadaraka kwani huzimwa na watu wenye asili ya maji, watu hawa hutumia nguvu nyingi katika utafutaji wa pesa kwani wanapokosa pesa huwe ni wenye huzuni sana na ni watu wenye kujikweza wanapopata pesa na ni watu wenye kupenda kuwakosoa wenzao pasipo wao kukosolewa, watu hawa ni wenye bahati ya kupata wapenzi wenye umaarufu, usomi, utafutaji.
Ila wanawake wenye asili hiii ya moto huwa ni watafutaji na washindani na wenza wao au marafiki zao na huwa wanapata na huwa hawakubali kushindwa hili pia ni hatari kwao kinyota kwani mwisho wao hupata maradhi yatokanayo na damu na watu hawa wapenzi wao ni watu wenye asili ya upepo.
Watu hawa maadui wao wengi ni watu wenye asili ya maji na utafutaji wao na maradhi yao huwa ni yenye asili ya udongo ndio maana huchoka sana baada ya shughuli zao na maungo yao kuuma kuanzia kichwani, mgongoni, mbavuni, mabegani.
Madini yao ni madini yenye aasili ya moto mfano chuma, bati na dhahabu na vito vyao vingi vyenye asili ya wekundu rangi ya moto, rangi ya safaya na rangi ya orange na wanashauriwa kwenye majumba yao au vitu vyao wapakae rangi zinazofanana na hizo na sadaka zao nyingi ziwe zina asili ya kuchinja hasa wanyama wenye asili ya wekundu madume na kahawia madume na nyota zao ni nyota za punda, simba na mshale, siku zao nzuri huwa ni jumanne, alhamisi na jumapili, vyakula vyao viwe ni vyakula visivyo ondolewa kiiini wajiepushe kula vyakula visivyokuwa na radha na mafusho yao ni kisti, sandarusi na udi uliochanganywa na kafru wapende dawa zenye asili ya kuchomwa zitawasaidia sana wasipende kuishi karibu na maji au sehemu yenye machimbo machimbo hayo ni maelezo kwa ufupi tu.
 Watu wenye asili ya hii kwa mwaka huu
Watu wenye asili hiii ya moto kwa mwaka huuu wamejikuta wakiahangaika sana katika utafutaji wa mali na kazi pasipo faida yoyote na wapenzi wao wamejikuta katika hali ngumu ya kimaisha na wamejikuta maadui zao ni wale wanawake wanaoshirikiana na mabosi zao kwahiyo wana uzito katika maswala yao wanashauriwa wasikate tamaa kwani mwaka unaokuja ni wafaraja kwao, mambo yao yatakuwa yana nafuu kwanzia mwezi wa sita mpaka wasaba au watakapotembelewa na mtu mwenye uso wa duara na mwenye misuli na mwenye kutumia vitu vyenye asili ya moto moto na watu wenye asili hiii hasa wanaume wako kwenye hali ngumu ya kimaisha kwa sasa, anapigishana kelele na mpenzi wake mwenye asili ya kuongeongea sana na watu hawa wamekutwa na matatizo ya msiba au ugonjwa kwa watu wa karibu wao kwa mwaka huu wa 2011 na mpaka sasa hawajapata suruhisho la matatizo yao na walipo sasa wanatafuta msaada kwa watu wa karibu wao pasipo mafanikio makubwa.
Watu wenye asili hii kwa mwaka 2012
Ni mwaka wa faraja kwao haswa unapofika katikati ya mwaka huo na wanashauriwa waende safari zao kwa upande wa mashariki na waondoke wakati wa mvua kuisha na wasikimbilie sehemu zenye mvua nyingi hawatafanikiwa wachanganyikane na watu wengi watapata msaada ni wakati mzuri kutumia malizao watafanikiwa au kuomba msaada kwa watoto wao na nchi zenye asili hiii ni wakati mzuri wa kujipanga kwa vita kwani watashinda,
Na tunatabiri 2012 nchi za mashariki zitaendelea kupata milipuko na jua kuwa kali na kutasikika habari za matajiri au watoto wa wakubwa kuchukua madaraka au makaimu wa viongozi wa sasa kuchukua madaraka au vyama vyenye asili ya jina linaloanzia na herufi O au zenye mgombea mwenye uso wa duara au mwenye nywele nyekundu au mwenye kipara katikati ndio watakao chukua uongozi, baadhi ya nchi zitajipanga kijeshi na zitatishia uvamizi na kutakuwa na visasi vya kifamilia, kinchi, kikabila na kidini, Kutakuwa na mkutano wa baadhi ya nchi kutaka kujitenga na kuanzisha majeshi yao na ajali nyingi zitakuwa za mlipuko kwa nchi za mashariki, mvua zitakuwepo na kutakokea mafuriko katika nchi zenye wanyonge wanyonge.





Monday, November 28, 2011

Maana ya Astrology (Elimu ya Unajimu)

Astrology (Elimu ya Unajimu) ni elimu inayohusiana na mwenendo na tabia za viumbe hai na nyota pamoja na anga. Elimu hii ni elimu inayotaka kuhusiana au kuendana na elimu astronomy ila utofauti wake ni kuwa astrology inaelezea sana mwenendo wa viumbe hai kwa ujumla na inahusisha viumbe hai na anga, ila elimu ya astronomy inaelezea elimu ya anga peke yake.

Kwa maana hiyo manajimu wanaamini elimu ya anga ambayo ni nyota,sayari na mwezi zina uhusiano wa kitabia,kiasili, kimaumbile,kimaisha ,kimali,kimaradhi,kitiba na kifo na kimajira ya sayari ya dunia na vilivyomo.
Astrology ni neno la kigiriki lenye maneno mawili yaliyo ungana yenye maana, astro ni anga na logy ni viumbe hai.

Nini Asili yake?
Baadhi ya dini na makabila wanahusisha elimu hii na utawala wa miungu yao au mizimu yao kiujumla zote hizo ni imani tu kwa jinsi wanavyoamini wao.
Elimu hii ina uhusiano na uumbaji wa mwenyezi mungu mmoja ambaye ni yehova, allah (s.w), aliumba kila kitu kwa mahesabu kwa hiyo mahesabu haya yalitumiwa na mwenyezi mungu. Wanajimu wanaamini hesabu hizi zina uhusiano na elimu ya unajimu.

Je ina uhusiano gani na mienendo ua kishetani?
Watu wengine wanaamini elimu hii ni mienendo ya kishetani kitu ambacho si kweli, elimu hii haihusiani na kishetani ila baadhi ya mila, makabila fulani za watu fulani zikiwepo za kidini na za kikabila huipelekea hii kwenye maswala ya kishetani.

Mahusiano katika uumbaji wa mungu.
Jehova ambaye ni mungu aliumba vitu hivyo kutoka  katika asili yake yeye, asili ya kila kitu ni moja ambayo ni yeye mwenyewe. Yehova aliumba vitu vinne ambavyo ammbavyo vitu hivyo vikatoa asili ya vitu vyote katika ulimwengu ambayo ni
Moto ambao aliuweka upande wa mashariki, Upepo ambao aliuweka upande wa kaskazini, Udongo ambao aliuweka upande wa  magharibi na maji ambayo aliyaweka upande wa kusini.

Uumbaji huuu ni kwa mujibu wa elimu ya unajimu kwa hiyo kila kitu katika ulimwengu huu wakiwepo malaika, majini, binadamu, wanyama, mimea, bahari, anga, ardhi, mbingu, jua, mwezi vyote vinatokana na hii asili nne.
Asili hizi nne ziliweza kuzaa asili saba na matawi yake mawili ambayo mungu aliumba mbingu saba, ardhi saba, bahari saba, mabara saba, sayari kubwa zipo saba, kwa hiyo inaaminika vitu hivyo saba vinatokana na  asili hizo nne.