Karibuni katika blog ambayo itakuwa inaelezea mambo ya kinajimu (astrology), mawe ya bahati ya kinyota, matukio kinyota na kiutabiri, matukio kimataifa na kimataifa na wanaopenda kujifunza elimu hii, mafusho,kuongelea viumbe kama majini, malaika, mizimu, freemason na iluminat, tiba kwa njia ya vyakula na matunda, magonjwa kinajimu na tiba zake.

Wednesday, December 7, 2011

Watu wenye asili ya udongo na tabia zao

Watu wenye asili ya udongo na tabia zao  April 20 - May 20, Augost 23 - September 22, December 22 - January 19, na Majina yanayoanziwa na herufi B, N, Z, F, R, J, V, au waliozaliwa tarehe 1, 6, 10, 14, 18, 22, 26, 30 au watu wenye mikono yenye nguvu, maumbile makubwa ya kimwili watu wenye miraba minne na wenye rangi ya kuteleza na wenye mikono na miguu bapa, na watu wenye rangi ya chocolate au wekundu wa chocolate. watu wa asili hii wanatabia ya utulivu pasina papara na utaratibu pasi na haraka, wapole mbele ya macho ya watu na wenye tabia ngumu kiusiri, watu hawa hawaonyeshi uasilia wao mbele ya macho ya watu, watu hawa wakiwa wanaume sio waongeaji sana tofauti na wanawake wa asili hii, mara nyingi wanawake wa asili hii huongea kwa kudeka, watu wenye asili hii hupenda kujifanya wanaelimu au matajiri hata kama hawana elimu wala utajiri na wanapenda marafiki wenye pesa, watu hawa mara nyingi wanafanya kazi ngumu na nzito na wanapenda kujitegemea pia watu hawa wanabahati mbaya ya kuachwa upweke na familia zao au kufiwa na wazazi wao, watu hawa hupendwa na wazazi wa kike, watu hawa hupenda ufuska wa chini chini na huwa hawajali lolote  wanapopenda, wanatabia ya kuugua ugua mara kwa mara na wakati mwingine hupenda kubadilisha dini zao au makabila yao au mila zao, watu hawa huwa wazembe wanapopenda ila mungu aliwajalia kuwa watu wenye nguvu katika maisha, hupenda kufikiri jambo kabla hawajaliamua hata kama uamuzi wao sio sahihi, watu hawa hawapendi ubishani hata wakijua unakosea wanakuacha na ujinga wako. Watu hawa hufanya kazi pasipo maneno mengi wanabahati mbaya ya kupata wapenzi mapepe na waongeaji hovyo, katika maisha yao watu hawa hukumbwa na mitihani mingi sana pasipo msaada wa ndugu au mtu yeyote hii huwafanya kujenga chuki na ndugu zao na kuamua kuishi peke yao pia watu hawa hupenda kujitegemea wao pasipo kutegemea, watu hawa huwa hawadumu na mpenzi mmoja ila mara nyingi huwapenda wapenzi wao wa mwanzo au waliowasaidia japo hupata nao migogoro mingi, hukumbwa na kashfa katika maisha yao za ubakaji, ulevi, uzinzi, wizi, ubakwaji hii huwa haribu sana kisaikolojia, watu hawa hupenda kufanya mambo yao kisiri siri na huwa sio wakweli na huwa hawakatai mapenzi wanapo tongozwa na ni watu wanao kaa na ashki sana pasipo kuonyesha, watu hawa hupenda kuingiliwa kimaamuzi na watu wenyine kwani huonekana ni wazembe hawana fikra zozote, pia wana bahati ya kung'ang'ania penzi lisilokuwa na ukweli na pesa zao nyingi huwa ni za msimu na watu hawa hupenda kusema na nafsi zao pasipo kuwaambia watu wengine na hawapendi kupaparikia mambo hata kama wanayapenda, watu hawa huwa na mitihani mingi sana lakini wanapata bahati sana na watu hawa hawaoni hatari kugombana na wazazi wao kwaajiri ya wapenzi wao na pia watu hawa huwa wavumilivu sana wakati wa shida, Watu hawa hawapendi vurugu na wanapochokozwa wana nguvu na mabavu sana pia watu hawa wana maamuzi yao pasipo kushirikisha watu wengine, Kazi zao nyingi huwa za asili ya upepo, wana kazi nyingi za mkono kama uchoraji, uandishi, upiganaji, uanajeshi, uchezaji wa mpira na michezo kwa ujumla na hupenda kazi za ofisini na wanabahati ya kupata kazi hata kama hawana elimu,watu hawa hujikuta wanfanya kazi hata kama hawana hobi nazo, pia watu hawa hawaamini maswala ya uchawi, dini zao, mila zao mpaka yanapowakuta matatizo na watu hawa hupenda kutumia dawa sana wanapokutwa na maradhi, na watu hawa kimapenzi wana nguvu za ajabu na huwa hawapendi kujisifia huonyesha matendo katika mapenzi, hupenda kuchezeana chezeana na wapenzi wao,
Madini yao ni shaba,petrol, ngozi, au vitu vinavyooshwa na petroli, madini ya risasi na fedha na rangi zao za kinyota ni nyeupe, kijani kibichi, udhurungi, nyeusi kwa watu wa nyota ya mbuzi, mafusho yao ni mushtaka, kachiri, miatisaila, siku zao ni ijumaa, jumatano na jumamosi maradhi yao ni mgongo, misuri, miguu kwenye vifundo, kifua, tumbo kujaa gesi, figo au ini, na nyota zao ni ng'ombe, mbuzi, mashuke na maadui zao ni watu wenye asili ya moto na upepo na wapenzi wao ni wenye asili ya maji na hayo ni kwa ufupi tu.
Watu wenye asili hii kwa mwaka huu.
Wamejikuta wakishughulika na mambo mengi ya kimaisha na mwaka huu umekuwa hauna heri wala shari japo wengine wamefukuzwa kazi au wameachwa na wapenzi wao, na mwishoni mwa mwaka huu wamejikuta kwenye matatizo na malumbano ya kifamilia au kikazi kwani baadhi ya watu wao wengine humpenda wangine hawampendi hujikuta wanaingilia penzi au wameingiliwa penzi na watu wakaribu yao ila akili zao zinawatuma kutafuta maisha pasipo kujali ndani ya nafsi zao .Sasa hivi nafsi zao zinasema hatama ya maisha yoa na hapo wanatafuta jambo wanahisi wakilipata wanahisi watapata nafuu ya maisha kwani wanaahidiwa mambo mengi na jamaa zao, kwa mwaka huu wamepata habari za harusi za ndugu zao au jamaa zao pia wanafikiria kuhusu watu aliopotezana nao miaka miwili mpaka minane iliyopita watu hawa wamepotezana nao au wamefariki, au wamefilisika kwani watu hawa walikuwa wakiwapa msaada,  Watu hawa wanabahati ya kuwa watu wazuri wanashauriwa kwa mwaka huu kuwa makini kwani ndipo faraja huja.
Watu wenye asili hii kwa mwaka 2012.
Wanajikuta bado wanatafuta  msaada kwa ajili ya matatizo yao lakini nawatabiria watakua ndani ya mitihani miziti bado na watashirikishwa kwenye mambo yasiyo wahusu, na wataendelea kupata taarifa za harusi pia watafiwa na rafiki au jamaa wa karibu au bosi au mfanyakazi mwenzao na mwaka huu ukifika katikati watapata nafuu ya maisha yao ila wawe makini kwani watapata maradhi ya miguu, wenye ndoa zao waendelee kuwa na ndoa zao wasiziache pia wanawake wa nyota hii wawe makini kwani wapenzi wao wanataka kuongeza, wake wengine, wanashauriwa kuwaona wataalamu wa kinyota kuwatengeneza au wakidini ili kuwaombea kuwaweka sawa kinyota pia kuna uwezekano watu wa asili hii kukutana na wapenzi wapya japo kutakuwa na kelele kutoka upande mwingine.
Nchi zenye asili hii kwa mwaka huu, ni nchi kubwa zitajikuta zikiwa bado katika vita na barozi zao kushambuliwa zaidi na watajikuta katika malumbano ya kisiasa na wananchi wao baadhi ya nchi hizi zitakumbwa na ukame, na nchi hizi zitatoa tamko la kugundulika dawa au tutatua matatizo ya kijamii na kuna kiongozi mkubwa katika nchi au serikali kufariki kwa ajali au maradhi ya muda mrefu na uwezekano wa mwanamziki au mtu maarufu kufa na habari hizo zatazagaa mashariki na magharibi na nchi hizi zitapata majibizano na nchi za mashariki na kuna kiongozi wa nchi kubwa atapata maradhi au kufa na ni wakati mzuri kwa nchi hizi kusaidia nchi zilizo chini yao kwani zitawafanya wapate nguvu zaidi kuna uwezekano mkubwa wa chombo cha usafiri kupotea au kuanguka au kuzama sehemu yenye maporomoko au milima mikubwa, na nchi hizi zitaweza kuzuia mashambulizi makubwa katika nchi zao.

Saturday, December 3, 2011

Watu wenye asili ya maji na tabia zao

Watu wenye asili ya maji na tabia zao June 21 - July 22, October 23 - November 21, February 19 - March 20, Majina yanayo anziwa na herufi D, P, H, T, L, X, na watu waliozaliwa tarehe 4, 8, 16, 12, 20, 24, 28 au wenye shepu zifuatazo, shepu za duara au za mraba, pua ya duara au watu wenye matatizo ya tumbo, watu hawa ni watu wenye akili sana na ni watu wenye kusoma sana, kutunza na kuhifadhi mambo kwa muda mrefu wenye kupenda kukaa na mizigo, ni watu wenye kupenda mashindano, wenye vigeugeu sana,wenye kulaumu laumu sana na ni watu wenye hisia na kuhisi kitu kikawa wawe makini na watu hawa kwani watu hawa wakikusemea jambo huwa, Watu hawa huanza bahati ya kupendwa na watu utotoni na mabibi zao, shangazi zao, wajomba zao, wazazi wao na watu hawa hujihisi ni wenye bahati sana na wazazi wao huhisi kuwa watu wa asili hii watakuwa wanategemewa kwasababu ya bahati zao za utotoni, wanapofikia baleghe huanza kukutwa na matatizo lakini ni watu wenye sifa ya kuwa na elimu katika familia zao watu hawa pia hugeukwa na watu wanao wategemea na pia huwa wana ugomvi na ndugu zao hasa wakike na  pia hulaumiwa kwa ugomvi kwani ni watu wenye kelele, watu hawa pia wana tabia ya kuto kuwapenda watu wenye kimbelembele, hupenda kuingilia kazi za watu kwani hujiamini wanaweza kufanya shughuli hizo na watu wenye kuchemsha akili sana kwenye shughuli zao pia watu hawa tabia zao ni zenye kubadilika badilika kutokana na watu wanaokutana nao, wanapenda kuwaamrisha wenzao na wanapenda kuwamiliki ndugu zao hasa wakike wanaofuatana nao na hilo huwaletea matatizo na ndugu zao hao.  Hawa hujifanya au huonekana na elimu hatakama hawana elimu, watu hawa ni waongeaji pindi unapo wazoea pia watu hawa ni wakali kwenye pesa na hujifanya hawana pesa hata kama wanazo huwa wanatabia ya kushindana na wapenzi wao, pia wanabahati ya kupendwa na wapenzi wenye pesa lakini hujikuta wanaangukia kwa wapenzi mafukara na mara nyingi maradhi yao mengi ni ya tumbo na moyo kupiga na pesha kushuka wanapopata matatizo au habari mbaya na pia wanabahati ya kusikilizwa na mzazi wa kike na hii huwakera ndugu zao na wanabahati ya kupendwa na mabosi wao wakubwa na hii huwakera wafanyakazi wenzao, watu hawa hupewa sifa ya ufitinishaji, utapeli, uongo na ni watu wenye makusudi makusudi na wanaume wenye nyota hii huonekana mazoba na matapeli japo huonekana tofauti na wanawake wa nyota hii. Wanapenda kusimamia shughuli za kifamilia na mwisho wa shughuli hizo hawapati sifa ila lawama.
Wanawake wa nyota hii huwa watafutaji na washindani wa kimali na watu wenye asili ya moto na watu hawa huwa na wasiwasi wa kuibiwa pia huwa ni wepesi wa kulia wanapo jitetea na watu hawa huwa na nguvu ya kushinda kesi hata kama wao wamekosa wanashauriwa kukaa na wapenzi wenye kumcha mungu kwani hii huwasaidia kukaa sawa, wanawake wanabahati ya kuolewa na wanaume weusi au wenye sura mbaya au wasiokuwa na mvuto, ni watu wenye kuakaa na kazi zao wenyewe kwa muda mrefu kwani wapenzi wao ni wenye nyota ya udongo na hukumbana na matatizo wanapofunga ndoa kuanzia siku mbili, wiki mbili, miezi miwili, miaka miwili na pia wanaume wa asili hii wanabahati ya kuoa wanawake wanowazidi umri, weusi au wenye sura isiyokuwa na mvuto na wanawake huwa ni wataratibu sana watu wa asili hii hupenda kufanya mapenzi kwa muda mrefu ndio maana huwa penda watu wenye asili ya udongo kwani mambo yao ni taratibu na wanaweza kuwahimili watu wa maji, wanashauriwa waoge kabla ya kukutana na wenza wao na wanatakiwa wao wawaanze wapenzi wao kwani wapenzi wao ni watu wa taratibu na wazito wazito na watu hawa wanashauriwa wapunguze lawama kwa wapenzi wao. wanashauriwa wawachezee wapenzi wao sehemu za shingo,tumboni, mapajani, wataniane na wapenzi wao na wanapotaniwa na wapenzi wao huwa ni wenye kusitasita na kukataa na mapenzi yao mara nyingi wayafanyie pembezoni mwa kitanda au kwenye kochi au kiti na wapende kutandika mavazi makubwa ya rangi ya nyota zao wawaeleze shida zao wapenzi wao baada ya kukutana nao na hii ni kwa ufupi tu. Kazi za watu hawa ni uhaziri, uhasibu,uuguzi, utumishi wa umma, ualimu biashara ya vyakula na masoko na biashara za kuhudumia watu kwa ujumla.
Madini yao ni madini ya fedha, aluminium na chuma na rangi zao ni nyeupe na nyekundu kwa watu wa nyota ya nge na nyota zao ni kaa, ngee na samaki wanashauriwa kula vyakula vyenye asili ya weupe na matunda yasiyokuwa na radha na vitu vyenye maji mengi, mafusho yao ni ubani maka, udi kafru, sandari ahmari na namba zao nzuri za bahati ni 4, 8 na 12,  siku zao ni jumatatu,jumanne na alhamis na mawe yao ya bahati yana asili ya weupe na damu ya mzee.
Watu wenye asili hii kwa mwaka huu.
Watu wenye asili hii kwa mwaka huu wamekutana na matatizo mengi ya kuchukuliwa wapenzi wao na ndoa zao kuingia matatizo na kugombana na baadhi ya ndugu na shughuli zao kuwa katika hali ya kati na kati na sasa wanawapenzi wa nnje kama kisasi kwa wapenzi wao na wapenzi ambao wako mji mwingine au upande mwengine na hao wapenzi wao wanawake wengine au familia nyingine, mwaka huu wamesherekea harusi za ndugu zao wakaribu na watu hawa wameenda miji mingine au sehemu zingine kutafuta msaada wa kitiba kwani mwaka huu wameandamwa na maradhi ya tumbo na miguu na hivi sasa wanampango wa kuishi kipeke yao peke yao na familia zao kwani wanajihisi ni wenye mikosi na kuonewa na mwaka huu wamejikuta wakipata habari za mapenzi sana yawe ya shari au ya heri na baadhi ya shughuli zao walizisimamisha kwa muda ila muda si mrefu watapata kazi katika sehemu zenye kuhudumia hudumia au biashara hii ni kwa ufupi tu
Watu wenye asili hii 2012.
Bado watakuwa kwenye mitihani kwa kipindi kifupi, ila maradhi yao yatakuwa katika hali ya kuondoka wanashauriwa watafute watu wa kuwasaidia, kwa mwaka unaokuja watapata utatuzi au watoto, mali au kazi mpya na wapenzi wao kuomba kurudiana nao na ndio mwaka wa kutoa tamko lao ila wawe makini kwani wanaweza kuhamishwa sehemu za kazi zao au kulipwa mafao yao au kuhama majumba wanayoishi na wanashauriwa kukaa na watu wenye asili ya moto kwani watu wamoto ndio mwaka wao wa kutawala, wajihadhali sana kujibu majibu ya dharau kwani ni wakati wa maadui zao kujipanga, mwaka huu watakutana na watu maarufu au kupata msiba mkubwa wa kifamilia hasa mwenye asili ya kike au mwanaume wenye umaarufu katika familia na zitasikika habari za uongo kuhusu wao wanatakiwa wajipange na wao pia ila kwa siri pasipo kusema na mwaka mzuri wa kutafuta pesa na watafanikiwa na wapenzi wao watapata matatizo ya kifedha, na watu hawa watapata elimu au kutembelewa na watu wajuzi.
Nchi zenye asili ya maji zitakumbana na lawama au maneno na yataendelea kukataliwa  mambo yao wanayoyafanya na nchi zingine watajikuta kwenye malumbano ya kisiasa katika nchi yao na baadhi ya viongozi wao kutaka kujiuzulu au kujiuzulu na baada ya matatizo hayo itakuwa faraja kwao na watapata msiba wa kiongozi wao mkubwa mwenye matatizo ya miguu na moyo au mwanamke mkubwa katika serikali na vifo hivi si kwa nchi hizi tu ila kwa ulimwengu mzima na litatokea tamko kubwa katika nchi hizi litakalo washangaza watu na kuwasikitisha au kuwafurahisha jambo hili litasababisha maandamano na marumbano na mikusanyiko ya watu na hii ni kwa ufupi tu.